UNHRC:Idadi ya wahamiaji imeongezeka maradufu
Posted by Unknown on 12:06 with No comments

Mashirika mawili ya kimataifa yanasema idadi ya wahamiaji wanaoingia Ulaya kupitia njia zisizo halali za kupitia pwani ya Mediterranea kufikia sasa imepita laki moja mwaka huu .
Mashirika hayo mawili UNHRC na lile linalohusika na wahamiaji IOM yametoa takwimu hizo zinazofanana kwa idadi ya wahamiaji wanaofikia kwanza Uitaliano na kisha Ugiriki.
IOM inasema takwimu hizo zaonesha ongezeko maradufu ikilinganisha na idadi ya wahamiaji mwaka uliopita wa 2014.

Aidha mashirika hayo yameonya kuwa idadi kubwa zaidi ya wahamiaji wanatarajiwa katika miezi ijayo.
Wengi wa wahamiaji wanaofikia kwanza Italia wanatokea Eritrea huku wale wanaofikia kwanza Ugiriki wanatokea Syria na Afghanistan.
Categories: NEWS
0 comments:
Post a Comment