Mfumo mbovu wa uteuzi chanzo cha matatizo CCM

Posted by Unknown on 17:15 with No comments
Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete akitangaza matokeo katika Mkutano Mkuu wa CCM uliopita
Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete akitangaza matokeo katika Mkutano Mkuu wa CCM uliopita
BAADHI ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM wameulalamikia mfumo wa uteuzi ndani ya chama hicho na kudai kuwa ni mbovu na umekisababishia chama hicho kujikuta katika matatizo.
Hali hiyo inadaiwa kuwafanya wanachama wengi kuhamia katika vyama vingine vya viasa ambavyo ni vya upinzani wakiwemo viongozi wa juu wa chama hicho.
Madai hayo yanakuja wakati ambapo chama hicho kimeingia katika kampeni zake za kuelekea uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani baada ya kukamilisha baadhi ya taratibu za uchaguzi mkuu.
Mgombea udiwani, Oneasmo Nywage katika kata ya Pandambili (CCM) akikiri uwepo wa mapungufu kwa baadhi ya wanachama licha ya chama hicho kujiwekea sera na taratibu nzuri.
Naye katibu wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wilaya ya Kongwa, Monica Nyabu yeye anataja baadhi ya masuala ya kupewa kipaumbele pindi uongozi mpya utakapoanza kazi baada ya uchaguzi mkuu.
Hayo yote yalibainishwa wakati wa mgombea udiwani, Onesmo Nywage akitangazwa rasmi kugombea nafasi hiyo kupitia chama cha Mapinduzi (CCM) kama mgombea halali wa udiwani kwa tiketi ya chama hicho katika kata ya Pandambili baada ya kumalizika mchakato wa kura za maoni.
Categories: