Hiki ndo kisa cha cha P Square kuvunjika

Posted by Unknown on 13:13 with No comments

Baada ya kudumu kwa kipindi cha miaka 19, kundi la P-Square limevunjika rasmi. Hakuna aliyewahi kuwaza iwapo kundi hili maarufu na lililofanikiwa kuliko yote Afrika lingeweza kufika katika hatua hii.
Wizkid_Psquare_Afrobeat_promo-0127
Ni hatua iliyowashtua wengi. Kwa sasa Paul na Peter Okoye ni wasanii wawili wanaojitegemea. Paul aka Rudeboy ameanzisha record label yake, Rudeboy Records, na Peter aka Mr P ametangaza rasmi uongozi wake mpya.
Nini chanzo cha ugomvi wao?
Inaonekana kuwa ugomvi ndani ya kundi hili ulikuwepo kwa muda mrefu na kwa kiasi kikubwa ulitokana na kaka yao Jude, kuwa meneja wao. Peter alihisi uongozi wa kaka yake uliokuwa wa kifamilia zaidi ulikuwa hauko sawa na alihitaji mabadiliko.
“A manager is been employed by the artiste not the other way round. #truthBeTold,” aliandika Peter February 17 mwaka huu katika mfululizo wa tweets kuelezea matatizo yao.
“People change management and you r not different. Usher Raymond did it,BeyoncĂ© did it as well. So it’s not new. Peter and Paul have the right to sack the entire management team. Business is Business. #Period. Been nurturing and managing these problems for over 4yrs now. Don’t take my silence as a weakness. #done,” aliongeza.
Mwanzoni alipigania kundi lao lisife lakini uongozi ubadilike.
“What the fans want is Peter and Paul Psquare and that’s what I want. Period! Psquare is not breaking up. But the management needs to go.”
Lakini inaonekana kuwa Paul hakuwa tayari kumtoa kaka yao Jude kama meneja wao. Na hiyo ndiyo sababu Peter ameamua kujiondoa kwenye kundi hilo. Mapacha hao walijikuta wakigawanyika na kurushiana vijembe February 18 kwenye Instagram. Paul alipost picha ambayo awali ilikuwa ikiwaonesha wao na kaka yao Jude, lakini akamuondoa Peter na kuandika:
This is where I belong and this is where I stand…….you do music in the studio, not on social media, you have family issues, you discuss that in close doors, not on social media ….. Family is family, blood is blood …. If you don’t do family business, then who am I to you?”
Kitendo hicho kilimuumiza Peter aliyejibu: And cutting me off from a picture and replacing me with a studio set says it all my bro. All because you want to sound matured and letting the pple insult and Laff at me. Peter Okoye the social media rant. I wish you well in all you do my bro. God bless our hustle.”
Mama yao angekuwepo yasingetokea?
Paul anaamini kama mama yake angelikuwa hai, yote yanayoendelea yasingetokea.
“Wish you were around, now I understand what these life is without having a mother, you’ve played your part thank you very much mum, miss you,” aliandika Paul kwenye picha ya marehemu mama yao aliyoiweka Instagram.
Mashabiki wameuamia lakini inabidi waukubali ukweli kuwa kundi hilo lililoiteka Afrika kwa kishindo kwa takriban miongo miwili limevunjika. Na sasa Peter na Paul wanaanza maisha ya solo huku Peter tayari akiwa ameanza kufanya show zake mwenyewe. Nani atafanya vizuri zaidi ya mwenzake? Muda utaongea.
Categories: ,